Karibu kwenye mafundisho ya Zúme. Zúme ni neno la Kigiriki linalomaanisha “chachu.”
Yesu anatuambia kwamba Ufalme wa Mungu ni kama mwanamke ambaye alichukua kiasi kidogo cha “ Zúme” na kukiweka kwenye kiasi kikubwa cha unga uliokandwa.
Alipokuwa akichanganya, chachu ilienea hata unga wote ukachachuka.
Yesu alikuwa anatufundisha kwamba mtu wa kawaida anaweza kutumia kitu kidogo sana na kusababisha kishindo kikubwa sana!
Ndoto yetu ni kufanya yale Yesu alisema -- kuwasaidia watu wa kawaida duniani kote kutumia vifaa vidogo kutoa vishindo vikubwa katika Ufalme wa Mungu!
Maagizo ya Yesu ya mwisho kwa wanafunzi wake yalikuwa rahisi. Alisema -- Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi –enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwa batiza kwa jina la baba, na la Mwana, nala Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Maagizo ya Yesu yalikuwa rahisi –Mkawafanye Wanafunzi
Amri yake jinsi ya kutekeleza hayo ilikuwa rahisi – mkafanye wanafunzi popote muendapo
Kwa hivyo ni hatua zipi za kuwafanya wanafunzi?
Kwa vile kitu kimoja alichoamuru ni kufanya wanafunzi, hiyo inamaanisha kila mwanafunzi anayemfuata Yesu anastahili kujifunza jinsi ya kutengeneza wanafunzi pia.
Hao wanafunzi wanastahili kutengeneza wanafunzi. Na hao wanafunzi nao wakatengeneze wanafunzi, pia.
Kuzidisha wanafunzi. Hivyo ndivyo Zúme inafanya kazi.
Ni kama chachu – ilijichanganya ndani mwa unga uliokandwa hadi wote ukawa chachu.
Wakati Yesu alipotoa amri hii ya kwenda kuwafanya wanafunzi, alitoa ahadi pia.
Yesu alisema – Nitakuwa nanyi daima. Hata ukamilifu wa dahari.
Kila mfuasi wa Yesu anapaswa kuzingatia ahadi ya kuwa Yesu yu pamoja nasi. Kwa sababu Yeye yuko!
Lakini pia inamaanisha kila mfuasi wa Yesu anapaswa kujitoa kwa ukweli kwamba Yesu anataka kila mmoja wetu atengeneneze wanafunzi. Kwa sababu Yeye alifanya.
Yesu alisema – nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi enendeni mkawafanye wanafunzi.
Mamlaka ambayo Yesu hutegemea wakati Anatutuma - ni mamlaka Yake
Yesu anasema hakuna mamlaka iliyo juu kuliko hiyo. Hakuna utamaduni uliyo na mamlaka zaidi.
Hakuna utamaduni uliyo na mamlaka zaidi. Hakuna sheria duniani iliyo na mamlaka zaidi.
Yesu alisema – nendeni mkawafanye wanafunzi.
Na kama Zúme - chachu – tutaendelea kuenda na kukua hata kazi yote ikamilike.